Kwa upande wake Mchungaji Yohane Parkipumi wa Kanisa la Moraviani amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kudumisha amani na kutoa wito kwa viongozi wa dini kuendelea kuliombea taifa.
“Tunamshukuru Rais Samia kwa juhudi zake za kulinda na kuimarisha amani na ninawaomba wachungaji, mashehe na viongozi wa mila kuendelea kuliombea taifa hasa tunapoelekea uchaguzi mkuu mwaka ujao,” amesema Mchungaji Parkipumi.
Naye Sheikh Iddy Ngella amehimiza wananchi kutumia fursa ya amani iliyopo kukuza uchumi wa taifa.
“Mahusiano mazuri kati ya Tanzania na majirani zake yanayojengwa na viongozi wetu ni fursa ya kukuza uchumi. Wananchi wa Arusha na Tanzania kwa ujumla, tumieni amani hii kuboresha maisha yenu na ya taifa,” alisema Sheikh Ngella.
Viongozi hao wa dini wamewataka wananchi wote kuhakikisha wanahakiki na kuboresha taarifa zao kwa wakati ili waweze kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.