Tamasha la Fintech la teknolojia ya kifedha katika Afrika mashariki lilionza tarehe 13 juni mwaka 2025 katika ukumbi wa Julius Nyerere international convention center (JNICC), limeelezwa ndio tamasha kubwa zaidi Afrika mashariki linalokutanisha wakali wa teknolojia wa fedha kutoka nchi zaidi ya 70 Duniani na kuungana na jumuiya ya fintech na kujadili fursa mbalimbali zinazosaidia kukuza teknolojia ya kifedha pamoja na kuinua uchumi kwa njia ya teknolojia.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi mkuu wa kampuni ya Eastern Star consulting group bw. Deogratius Kilawe katika ufunguzi wa tamasha hilo.