NA EMMANUEL MBATILO
Katika hatua nyingine, Prof. Palangyo alieleza kuwa TIA inamiliki kampuni tanzu ya kitaalamu iitwayo Tanzania Institute of Accountancy Bureau (TIA Bure), ambayo imekuwa ikitoa huduma za ushauri katika masuala ya biashara, uhasibu na manunuzi kwa taasisi mbalimbali za umma na binafsi.
Kwa lengo la kuendelea kujenga mahusiano na jamii na kuonesha matokeo ya kitaaluma, TIA inatarajia kufanya Mkutano Mkubwa wa Kitaaluma mwezi Novemba 2025 mkoani Mwanza, ambapo wananchi watapata fursa ya kujifunza na kushiriki mijadala ya maendeleo.
Kwa mujibu wa Prof. Palangyo, Taasisi hiyo kwa sasa ina jumla ya wanafunzi zaidi ya 30,000, na inalenga kuongeza idadi hiyo ili kuendana na dira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuhakikisha elimu ya juu inawafikia wananchi wengi zaidi.