Nahodha wa Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars Mbwana Samatta ameandika rekodi mpya baada ya kujiunga na Le Havre ya Ligi Kuu Ufaransa Ligue1.
Samatta ambaye ameandika rekodi ya kuwa Mtanzania wa kwanza kucheza Ligue1 msimu wa 2025/26 anajiunga na Le Havre kama Mchezaji huru baada ya kumaliza Mkataba wake wa miaka miwili na PAOK ya Ugiriki.
Le Havre inakuwa Klabu yake ya sita Samatta kucheza soka katika ardhi ya Ulaya baada ya KRC Genk na Royal Antwerp za Ubelgiji, Aston Villa ya England, Fenerbahce ya Uturuki na PAOK ya Ugiriki