*Nchi inashuhudia mageuzi makubwa kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia.
*Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kinara wa nishati safi ya kupikia.
*Ubunifu wa teknolojia za nishati safi ya kupikia kusaidia kupiga hatua.
Kaimu Mkurugenzi wa Nishati safi ya Kupikia kutoka Wizara ya Nishati, Ngereja Mgejwa amesema Nchi inashuhudia mageuzi makubwa katika Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia nchini hii inasaidia katika kulinda afya, kutunza mazingira pamoja na ustawi wa jamii ambapo ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia Kinara wake ni Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Mgejwa aliyasema hayo tarehe 05 Aprili, 2025 Alipotembelea Chuo cha VETA Moshi, Mkoani Kilimanjaro kuona ubunifu wao wa Majiko yayanayotumia gesi pamoja na kuhamasisisha matumizi ya nishati kupikia na aliwapongeza kwa ubunifu wao ambao utasaidia kupiga hatua katika suala la zima la Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.
Ziara hiyo, inatokana na maelekezo ya Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko (Mb.), Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati alipokuwa Mgeni Rasmi katika
Maadhimisho ya Wiki ya miaka 50 ya utoaji Elimu na mafunzo ya ufundi stadi nchini (VETA) iliyofanyika jijini Dar es Salaam, tarehe 21 Machi 2025.
Aidha, Mgejwa alieleza kwamba lengo la Serikali ni kuona matumizi ya nishati safi ya kupikia yanapanda kufikia asilimia 80 ifikapo 2034.
Pia, alieleza matumizi ya nishati isiyo safi ya kupikia yanavyosababisha madhara ya kiafya, kimazingira na hata kiuchumi, huku akieleza takwimu ambazo zinaonyesha watu takribani 33,024 hupoteza maisha kutokana na matumizi ya nishati isiyo safi ya kupikia.
Kwa upande wa Mkuu wa Chuo cha Ufundi Stadi VETA Moshi Mha. Lupakisio Mapamba amesema ubunifu wa Teknolojia ya jiko linalotumia gesi litasaidia kuondokana na uchafuzi wa mazingira ikiwemo ukataji wa miti hovyo pamoja na kulinda afya kutokana na moshi pale unapotumia jiko la kawaida la mkaa au kuni.
Pia aliongeza kuwa majiko ya gesi yaliyobuniwa na Chuo Cha Ufundi VETA Moshi yataweza kuwarahisishia watumiaji kutumia bila kuchafua mazingira hasa katika suala la ukataji wa miti pamoja na kumkinga pale anapopika kwa kuwa jiko la gesi halitoi moshi hivyo hatuweza kudhurika kama atumiavyo majiko mengine”. Amesema Mapamba.