Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Mwajuma Waziri aongoza Menejimenti ya Wizara ya Maji na watumishi wa Sekta ya Maji katika sherehe za maadhimisho ya Sikukuu ya Wafanyakazi-Mei Mosi kitaifa 2025 yaliyofanyika mkoani Singida.
Mhandisi Mwajuma amekuwa mfanyakazi bora wa Sekta ya Maji na miongoni mwa wafayakazi 4 bora kutoka Sekta ya Maji kitaifa kwa mwaka 2025.
Maadhimisho hayo yenye kaulimbiu “Uchaguzi Mkuu 2025 Utuletee Viongozi Wanaojali Haki na Maslahi ya Wafanyakazi sote Tushiriki” yaliongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.