Waziri wa Maji Mhe.Jumaa Aweso akiwasilisha leo Mei 8,2025 bungeni jijini Dodoma makadirio ya Mapato ya Wizara hiyo kwa mwaka 2025-2026 .


Waziri wa Maji Mhe.Jumaa Aweso akiwasilisha leo Mei 8,2025 bungeni jijini Dodoma makadirio ya Mapato ya Wizara hiyo kwa mwaka 2025-2026 .
Na Alex Sonna-DODOMA
KATIKA mwaka wa Fedha 2025/26, Wizara ya Maji imejipanga kuhakikisha vijiji ambavyo havina maji vinafikiwa na vinakuwa na Maji.
Hayo yameelezwa leo bungeni Machi 8,2025 na Waziri wa Maji Jumaa Aweso wakati akiwasilisha makadirio ya Mapato na matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026.
Waziri Aweso amesema
Wizara itaendelea na utekelezaji wa programu maalum ya kuhakikisha maji yanapatikana katika maeneo ya vijijini.
Aweso amesema Wizara imepanga kuendelea kutekeleza miradi 1,318 ya maji vjijini
Amesema kwa vijiji 1,781 ambavyo havijafikiwa imejipanga kuhakikisha inafikiwa na Maji.