Klabu ya Fountain Gate imetangaza kuandaa michuano maalumu ya PRE-SEASON INTERNATIONAL TOURNAMENT, michuano yenye lengo la kuzipa maandalizi mazuri timu za ligi Kuu Tanzania.
Timu zitakazoshiriki ni Fountain Gate FC, Dodoma JIJI, Tabora Utd, Coastal Union, JKU SC na CITY ABUJA FC.
PRE-SEASON INTERNATIONAL TOURNAMENT itaanza Agosti 31 na yataisha Septemba 06, mashindano yatafanyika katika uwanja wa TANZANITE KWARAA, BABATI.