Mwanariadha Alphonce Felix Simbu ashinda mbio za riadha za dunia ambazo zinafanyika jijini Tokyo, nchini Japani na kumshinda mpinzani wake kwa tofauti ya sekunde 0.03 ambaye ni mwanariadha kutoka Ujerumani Amanol Petros.
Alphone Simbu ameshinda mbio za dunia kwa kukimbia kwa saa 2:09:48 na kufanikiwa kupata medali ya kwanza ya dhahabu kwa Tanzania katika mashindano ya dunia ya Tokyo 2025 .