Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaani Jacobs Mwambegele (kulia) akizungumza na wananchi wa Mtaa wa Nyuki Kata ya Lukobe Manispaa ya Morogoro mkoani Morogoro wakati alipokitembelea kituo hicho cha ofisi ya Serikali za Mtaa kukagua zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura lililoanza Machi mosi na litafikia tamati Machi 07,2025. (Picha na INEC).
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaani Jacobs Mwambegele (kulia) akiangalia namna mwendesha kifaa cha Biyometriki (BVR) anavyochukua picha wakati alipotembelea kituo cha Mafiga B Manispaa ya Morogoro mkoani Morogoro kuangalia zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura lililoanza mkoani humo Machi mosi na litafikia ukomo Machi 07, 2025. (Picha na INEC).
Mwnanchi wakiwa wamejitokeza kwa Wingi katika moja ya vituo vya Kata ya Mafiga Manispaa ya Morogoro kwaajili ya kuajindikisha na kuboresha taarifa zao katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ambalo zoezi hilo linaendelea Mkoani Morogoro kuanzia Machi mosi hadi Machi 07,2025. (Picha na INEC).
……….