Aliyekuwa nahodha wa Simba Sc, Mohammed Hussein Tshabalala ‘Zimbwe Jr’ ametambulishwa kama mchezaji mpya ndani ya klabu ya Yanga Sc kama mchezaji huru baada ya mkataba wake na Wekundu wa Msimbazi, Simba Sc kufikia ukomo.
Tshabalala anatua Jangwani baada ya kuhudumu kwa miaka 11 ndani ya klabu ya Simba Sc tangu mwaka 2014 aliposajiliwa akitokea Kagera Sugar akiwa na miaka 18 tu.