Klabu ya Azam FC siku ya leo itakuwa uwanjani majira ya saa 10:15 jioni kusaka tiketi ya kufuzu hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika kwa mara ya kwanza.
Azam FC watakuwa ugenini dhidi ya KMKM ya Zanzibar katika mchezo wa mkondo wa kwanza ambao pengine ukawapa matumaini ya kuandika historia mpya kama watapata matokeo mazuri kabla ya mchezo wa pili utakaopigwa nyumbani.
Unawapa asilimia ngapi za ushindi Matajiri wa Chamazi katika mchezo huo ?.