Msajili wa Vyama vya Siasa, Mhe. Jaji Francis Mutungi,akizungumza wakati akifungua kikao cha dharura cha Baraza la Vyama vya Siasa kinachofanyika jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa Ndg. Juma Ali Khatibu,akizungumza wakati akifungua kikao cha dharura cha Baraza la Vyama vya Siasa kinachofanyika jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika akichagia mada wakati wa kikao cha dharura cha Baraza la Vyama vya Siasa kinachofanyika jijini Dodoma.
“Ni muhimu kwa vyama vya siasa na anaamini vyama vyote 19 vitashiriki na kuhakikisha uchaguzi unakuwa mzuri.
“Rai yangu kwa viongozi wa vyama vya siasa na viongozi wengine wa dini, mila tushirikiane kukumbusha watu wetu waende kujiandikisha hii ni haki ya kila mmoja bila kujali, chama au dini, kila mmoja ana haki ya kujiandisha na kwenda kushiriki uchaguzi, ,”amesema
Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa NCCR MAGEUZI Joseph Selasini bhui amesema Mkutano huo wa dharura ni wa kwanza kufanyika katika kipindi ambacho wanajipanga kuelekea kwenye uchaguzi wa serikali za mtaa.
“tunampongeza Msajili wa Vyama vya siasa kwa ubunifu huu wa kuwakutanisha viongozi wa vyama vya siasa na kujadili agenda moja tu ya hali ya Siasa nchini kabla ya uchaguzi ila kusaidiana katika kuwahamasisha wananchi kujiandikisha na kujitokeza katika uchaguzi, jambo hili hata Dunia itaona nia njema ya kutaka kuona uchaguzi unakuwa huru na haki, “ameeleza Selasini