Na. Mwandishi wetu – Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema serikali itaendelea kuwawezesha Wajasiriamali Wanawake na Vijana kwa kuwapatia maarifa, masoko, fursa za kijamii na kiuchumi ili waweze kupiga hatua katika kujenga uchumi wa familia na jamii kwa ujumla.

Mhe. Ridhiwani amebainisha hayo leo Novemba 13, 2024 Jijini Dar es salaam wakati wa hafla ya Panda event 2024, ambayo ilikuwa na kauli mbiu isemayo Wawezeshe Wasichana na Wajasiliamali kuvumbua fursa za masoko na kuboresha viwanda