Mwenyekiti wa Bodi ya Usimamizi na Utoaji wa Leseni kwa Wapima Ardhi (BCLS) ambaye ni Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Hamdouny Mansour akizungumza wakati wa kikao cha Bodi kinachofanyika jijini Dodoma kuanzia tarehe 18 hadi 19 Machi 2025.
Sehemu ya wajumbe wa Bodi ya Usimamizi na Utoaji Leseni kwa Wapima Ardhi wakiwa katika kikao cha bodi hiyo kinachofanyika jijini Dodoma kuanzia tarehe 18 hadi 19 Machi 2025 .
Mwenyekiti wa Bodi ya Usimamizi na Utoaji wa Leseni kwa Wapima Ardhi ambaye ni Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Hamdouny Mansour akisisitiza jambo wakati wa kikao cha Bodi kinachofanyika jijini Dodoma kuanzia tarege 18 hadi 19 Machi 2025.
Mwenyekiti wa Bodi ya Usimamizi na Utoaji wa Leseni kwa Wapima Ardhi (BCLS) ambaye ni Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Hamdouny Mansour akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa bodi wanaoshiriki kikao kinachofanyika jijini Dodoma kuanzia tarege 18 hadi 19 Machi 2025. (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)
………………….
Na Munir Shemweta, WANMM
Bodi ya Usimamizi na Utoaji wa Leseni kwa Wapima Ardhi (Board of Control and Licensing of Surveyors-BCLS) imeanza kikao chake cha siku mbili jijini Dodoma ambapo katika kikao hicho inajadili na kupitia masuala mbalimbali ikiwemo mashauri ya kinidhamu kwa makampuni yaliyokiuka maadili, Kanuni na taratibu za upimaji.
Moja ya jukumu la Bodi ya Usimamizi na Utoaji Leseni kwa Wapima Ardhi ni kusimamia utendaji wa wapima ardhi kwa lengo la kuongeza tija katika kazi za kitaalamu zisizohusiana na upimaji ardhi.
Aidha, katika kikao hicho kilichofunguliwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo Bw. Hamdouny Mansour tarehe 18 Machi 2025, mbali na kupitia mashauri ya makampuni ya upimaji yaliyokiuka taratibu, kikao pia kitapitia mitaala ya shahada ya GEOMATICS inayotolewa na Chuo Kikuu cha Ardhi.
Bodi ya Usimamizi na Utoaji wa Leseni kwa Wapima Ardhi (Board of Control and Licensing of Surveyors-CLS) imeanzishwa kwa sheria ya upimaji ardhi Sura ya 324 chini ya Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Baadhi ya majukumu ya bodi hiyo ni kusajili na kutoa leseni kwa wapima ardhi wenye sifa, kutunza rejista kwa wapima ardhi waliosajiliwa, kufanya mapitio na kutoa mapendekezo ya mitaala mipya na inayohusishwa na stashahada na shahada mbalimbali za vyuo vya kati na vya juu pamoja na kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya wataalamu waakaobainika kukiuka sheria, kanuni na miongozo mbalimbali ya upimaji.