……………….
Na Sixmund Begashe – Singida
Wataalam wa Sera na Mipango Wizara ya Maliasili na Utalii wameendelea na kikao kazi Mkoani Singida kwa lengo la kupata uwelewa wa pamoja wa namna bora zaidi ya utekelezaji wa mpango wa shughuli mbalimbali za Uhifadhi na Utalii kwa mwaka 2025/2026
Akizungumza kwenye kikao kazi hicho, Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango Bw. Abdullah Mvungi licha ya kuwapongeza wataalam hao kwa michango mizuri, amewasisitiza kuendeleza umakini katika mapitio na maboresho ya mipango hiyo ili iweze kuleta tija zaidi kipindi cha utekelezaji wake.
Bw. Mvungi ameeleza kuwa, wataalam hao kutoka Idara na Taasisi mbalimbali za Wizara hiyo wamekuwa ni chachu kubwa ya Maendeleo endelevu ya Uhifadhi na sekta ya Utalii kutokana na umahiri wao katika sera na Mipango inayotekelezeka katika Wizara hiyo yenye mchango mkubwa katika pato la taifa.