Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko leo 17 Aprili, 2025 ameshiriki Mkutano wa Mawaziri wa Nishati wa kikanda kwa nchi za Afrika Mashariki ambao ni wanachama wa Umoja wa Soko la pamoja la Kuuziana Umeme na Kuimarisha Mifumo ya Gridi ya EAPP (Eastern Africa Power Pool).
Mkutano huo wa siku 2 umeanza tarehe 16, Aprili 2025 na unatarajiwa kumalizika leo Aprili 17, 2025 jijini Kampala nchini Uganda