OR-TAMISEMI
Mkurugenzi wa Idara ya Afya Lishe na Ustawi wa Jamii , Ofisi ya Rais TAMISEMI, Dkt. Rashid Mfaume amesema mahusiano mazuri kati ya Serikali na taasisi za dini yamekuwa chachu katika kufanikisha utoaji wa huduma za afya kwa wananchi.
Dkt. Mfaume ameyasema hayo hivi karibuni mara baada ya kutembelea katika Hospitali ya Cardinal Rugabwa inayomilikiwa na Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam katika ziara yake inayoendelea mkoani huku yenye lengo la kuangalia upatikanaji wa huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii.
“Hapa tunaona mitambo kikubwa ya kutolea huduma za afya, Serikali imeiweka mazingira mazuri ya ushirikiano kati ya Serikali na taasisi za dini zote ikiwa ni pamoja na uwekezaji kwenye Sekta ya afya” amesema Dkt.Mfaume
Aidha, Dkt. Mfaume amezitaka timu za usimamizi wa afya (CHMT) katika Halmashauri kuendelea kufanya kazi kwa ukaribu na taasisi hizo kwa kuwa zinatekeleza majukumu hayo kwa niaba ya Serikali.
Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo Sr.Dkt. Sarah Deogratius amesema ziara ya Mkurugenzi katika Hospitali hiyo imewatia moyo wa kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi.