Watu wanaowapeleka madereva kufanya kazi nje ya nchi wanawajibu wa kufanya utafiti kujua mahitaji ya eneo wanaloenda ni yapi tofauti na mahitaji ya magari ya Tanzania.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe Profesa Adolf Mkenda amesema hayo jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio ya Wizara hiyo katika miaka minne ya serikali ya awamu ya sita.
Waziri Mkenda amesema wahitaji hao wa madereva wanatakiwa kujua aina ya magari yaliyopo Tanzania ni ya namna gani, yanayoenda Kongo ni ya namna gani, madereva wa Tanzania wanajifunza nini, hivyo mtu akiwachukua watu nchini na kuwapeleka Qatar ni vizuri kwanza akaangalie, asiwachukue na kuwakimbiza kule halafu wakaenda kupimwa hilo ni jambo la muhimu kulifanya.
“Lakini pia tuna haja ya kuwafundisha magari yote hata yale ambayo hayajaingia nchini lakini sisi tulishatoa maelekezo miaka miwili iliyopita kwamba Chuo cha Ufundi Arusha kiingie makubalianao na makampuni ya magari na tayari wameanza mazungumzo na wengine wanaingia mkataba lakini pia tulishawaambia VETA kufanya jambo hilo” Amekaririwa Prof Mkenda
Hata hivyo amesema hata kwenye magari wanahitaji siyo fundi Mechanical pekee bali wanahitaji fundi ambaye anajihusisha na shughuli zote za mfumo wa magari ya kisasa (Mechatronics).