Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation for Civil Society (FCS ),Justice Rutenge akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha leo


…………
Happy Lazaro ,Arusha .
ZAIDI ya Washiriki mia nane kutoka sekta mbalimbali wanatarajiwa kushiriki katika wiki ya azaki inayotarajiwa kuanza rasmi June 2 hadi 6 katika hoteli ya Mount Meru iliyopo jijini Arusha .
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha leo ,Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation for Civil Society (FCS ),Justice Rutenge amesema hii wiki ya azaki sasa hivi inafanyika kwa mara ya saba na walianza mwaka 2018 ambapo kwa mwaka huu wanatarajiwa kuwa na washiriki kati ya mia nane hadi mia tisa kutoka sekta mbalimbali.
Amesema kuwa ,kauli mbiu ya mwaka huu ni “Pathway to progress” ambayo inamaanisha tunapita njia gani ili tuweze kufika yale maono ya maendeleo ambayo tumejiwekea na wote mnafahamu kuwa mwaka huu tumeshuriki katika mchakato wa kutengeneza dira yetu ambayo itazinduliwa hivi karibuni.
Rutenge amesema kuwa dira hiyo imeweka malengo ya kuwa Tanzania iwe nchi ya uchumi wa kati ngazi ya juu ni maono makubwa hivyo lazima tukae chini tuangalie tunaweza kupita njia gani ya kufikia kwenye maono haya ambayo tumejiwekea.
Ameongeza kuwa,Tanzania ina “frame work” ambayo inaongoza jinsi ambavyo tunapanga maendeleo na maendeleo ambayo unaona sasa hivi yalipangwa miaka kadhaa iliyopita walikaa na kufanya kazi ya kutengenenza dira yao rasmi ya kwanza ya maendeleo na hiyo inakuwa dira yao rasmi ya pili ya maendeleo ambapo baada ya dira hiyo wanafanya kazi ramsi ya kutengeneza mpango elekezi wa muda mrefu .
“Sisi kama asasi za kiraia tumeshiriki kiasi kikubwa sana kwenye kuhakikisha kuwa dira pamoja na mpango elekezi wa muda mrefu unahakisi maoni ,mawazo,na matarajio ya wananchi na wamekuwa sehemu ya nafasi kubwa sana katika michakato hiyo miwili .”amesema Rutenge.
“Tunataka kutumia fursa hii kuendeleza ule ubia na ushirikiano ambao tumeanza katika kuangalia mustakabali wa Tanzania utakuwaje na tutachukua muda mrefu sana katika kuzungumzia dira ya maendeleo ya Taifa .”amesema .
Amesema kuwa, dira ya Taifa inahakisi pale wanapotaka kufika wao kama asasi za kiraia wapo kwa ajili ya kukumbusha umma wa watanzania kuwa maendeleo yanahusu watu na sio vitu watu ndio somo kubwa la maendeleo.
“Tutatumia muda mrefu sana pia kuzungumza kuhusu je mwanachi wa Tanzania ikifika mwaka 2050 anafananaje anakuwa na uwezo upi kama mwananchi anashirikiana vipi na serikali yake na fursa ambazo zinatokea katika sekta binafsi ikiwemo fursa za kidunia .”amesema Rutenge .
“Katika hilo kuna umuhimu mkubwa wa kuangazia sekta ya elimu ambayo itatusaidia katika kutupeleka katika maono ambayo tunataka kuyafikia ambapo sekta ya elimu nguvu kazi ya Taifa itakuwa ni muhimu sana ambayo wataangazia katika hii wiki ya azaki .”amesema .
Aidha amefafanua kuwa,WAZIRI wa nchi ,ofisi ya Rais (uwekezaji)
Profesa Kitila Mkumbo anatarajiwa kushiriki katika wiki ya azaki mwaka huu 2025 katika kuona asasi pamoja na wadau wengine watakavyoweza kuchangia katika ile dira ambayo tumeitengeneza pamoja .
Amesema kuwa, katika wiki hiyo ya azaki pia watatumia kama nafasi ya kujihoji na kufanya tathmini kama sekta ya azaki wapo wapi ,changamoto wanazopitia ni zipi ,wapi wanafanya vizuri wapi wanahitaji maboresho kwani sio kitu ambacho wanakiona sana kwenye sekta zingine na kuangalia jinsi gani wataweza kuendeleza mustakabali wa sekta hiyo kwani baada ya kuangalia mustakabali wa Taifa wataangalia pia mustakabali wa sekta yao ya azaki.
Mwenyekiti wa bodi ya FCS ,CPA Mercy Silla amesema kuwa wanajua mchango wa FCS na wao kama bodi wapo pamoja na wanachama na washiriki wote ambapo amesema maono yao wanatamani na wanaamini kuwa na raia ambao wanawezeshwa ambao wanajitegemea na wenye kuwajibika na pia wana haki zao za kijamii na za kiuchumi na kufurahia maisha bora.
Amesema kuwa,kila mtu anatamani hivyo na wao ndio tamanio lao kubwa .
Amesema kuwa ,tangu mwaka 2002 FCS wamekuwa wakitoa ruzuku ama kuwezesha asasi mbalimbali katika kuwafikia wananchi katika kusikiliza hoja zao na katika kuleta mabadiliko ya kiuchumi na kimaendeleo na wamefikia taasisi elfu sita na kazi kubwa imefanyika katika muda wote huo .
Silla amefafanua kuwa, umuhimu wa kuendelea kushirikiana na kuzisaidia asasi mbalimbali ili kuweza kuleta mabadiliko hayo kwa wnaanchi wetu .
Ameongeza kuwa wiki hii ambayo inakuja ni mategemeo yao kuwa kutakuwa na wadau mbalimbali kutoka asasi mbalimbali pamoja na taasisi mbalimbali kuweza kuleta mabadiliko ya kiuchumi katika kusikiliza mbalimbali .
Katibu Mkuu wa Baraza la Taifa la Mashirika yasiyo ya Kiserikali, Adamson Nsimba amesema kuwa, wanaangalia namna wanaweza kubadilisha swala la maendeleo ambapo mwaka huu wanaangalia katika dira huku akiyataka mashirika yote kufuatilia mjadala huo ili waweze kujitathmini na kwenda mbele zaidi .
Kwa upande wake Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa ASASI ya Tanzania Bora Initiative (TBI)Ismail Biro amesema kuwa mwaka huu wanaangalia umuhimu wa uwezeshaji mbalimbali wa mabadiliko kwani hilo ni jambo letu sote.
“Tunataka kuwa na nafasi nzuri ya kuweza kufanya tafakuri katika swala zima la uwezeshaji Tanzania katika swala zima la maendeleo katika kuhakikisha wanaungana pamoja ili mtanzania aweze kunufaika kimaendeleo. “amesema.