Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Hamza S. Johari amewasilisha Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa Mwaka 2025 (The Written Laws (Miscellaneous Amendments) Bill, 2025).
Mwanasheria Mkuu wa Serikali amewasilisha Muswada huo tarehe 5 Juni, 2025 katika Mkutano wa Kumi na Tisa , Kikao cha Arobaini cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linaloendelea Bungeni, Jijini Dodoma.