Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Bi. Martha Chassama amekutana na kuzungumza na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasilino wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA), Bi. Catherine Sungura na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Masoko wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Bw. Athumani Shariff katika kikao kifupi kilichofanyika jijini Dodoma. Kikao hicho kifupi kililenga kujengeana uwezo wa taasisi hizo hususan katika maeneo ya vijijini ili kuongeza chachu katika maeneo hayo.