GWARIDE Maalumu la Kikkosi cha FFU lililoandaliwa kwa ajili ya ufunguji wa Baraza la Kumi la Wawakilishi Zanzibar katika viwanja vya Baraza Chukwani Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Jijini Ungaja leo 23-6-2025, likitowa salamu ya heshima kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi.(Picha na Ikulu).
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akipokea salamu ya heshimam, wakati wa gwaride rasmin la Kikosi cha FFU lililoandaliwa kwa ajili ya ufungaji wa Baraza la kumi la Wawakilishi Zanzibar, ufungaji huo uliyofanyika leo 23-6-2025, katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Chukwani Wilaya ya Magharibi “B” Unguja Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikagua gwaride rasmini la Kikosi cha FFU lililoandaliwa kwa ajili ya ufungaji wa Baraza la la Kumi la Wawakilishi Zanzibar, lililofanyika katika viwanja vya Baraza Chukwani Wilaya ya Magharibi “B” Unguja Jijini Zanzibar leo 23-6-2027.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika paredi na Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe.Zuberi Ali Maulid, baada ya kulihutubia na kulifunga Baraza la Kumi la Wawakilishi Zanzibar,ufungaji huo uliyofanyika leo 23-6-2025 katika ukumbi wa Baraza Chukwani Wilaya ya Magharibi “B” Unguja Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu).