Na Sophia Kingimali.
Naibu waziri wa Wizara ya Nishati Judith Kapinga amelipongeza Shirika la umeme nchini TANESCO kwa hatua kubwa waliyoipiga ikowemo ya kutumia mifumo ya Tehama katika kuvutia uwekezaji wa miradi yake ya umeme.
Pongezi hizo amezitoa leo juni 25,2025 jijini Dar es salaam wakati akizindua mfumo wa usimamizi wa uwekezaji wa Tanesco (TIMS)wenye lengo la kusaidia na kuvutia uwekezaji kwa miradi mbalimbali inayofanywa na shirika hilo.
Amesema mfumo huo unaruhusu wawekezaji kujisajili na kuwasiliana na shirika katika kuingia ubia wa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya uzalishaji umeme.
“Uzinduzi huu ni utayari wa TANESCO kushirikiana na sekta binafsi ili kutekeleza miradi mikubwa ya uzalishaji umeme na tayari mpaka sasa tunapouzindua mfumo huu tayr miradi minne imeshawekwa kwenye mfumo”,Amesema Kapinga.
Aidha kapinga ametoa rai kwa wawekezaji nchini kuchangamikia fursa ya uwekezaji katika miradi ya uzalishaji umeme ya TANESCO.
Ameongeza kuwa mfumo huo ni mwendelezo wa safari ya kidigital ndani ya shirika hilo lakini utekelezaji wa maelekezo ya serikali ya kutaka matumizi ya mifumo inayosomana ili kurahisisha huduma na kuongeza ufanisi wa kazi.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Lazaro Twange amesema mfumo huo unafaida nyingi ikiwemo kuongeza uwazi,kupunguz urasimu kwa wawekezaji lakini utaongeza tija kwenye utoaji wa huduma.
Amesema pia mfumo huo wa TIMS utasaidia kupima jinsi shirika linavyotoa huduma na utasaidia taasisi kwenye uwazi na uwajibikaji.
“TANESCO ina ‘interest’ na uwekezaji nchini hata kuanzisha mfumo huu ambao umetengenezwa na wataalam wetu wa ndani ilikuwa hamu ya shirika lakini ni utekelezaji wa adhima ya serikali ya juhakikisha mifumo inafanyakazi katika kuvutia uwekezaji hivyo kupitia mfumo huu wawekezaji wataweza kupata taarifa zote za miradi yetu”,Amesema.
Akielezea mfumo huo Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa mipango,utafiti na uwekezaji CPA Renata Ndege amesema mfumo huo ni kuchocheo cha ufanisi na uwekezaji.
“Huu ni mfumo rahisi na umerahisisha mawasiliano kati ya wawekezaji na shirika lakini pia ni kichocheo cha kimkakati katika uwekezaji”,Amesema.