Watu kadhaa wanahofiwa kupoteza maisha baada ya kutokea ajali iliyohusisha basi la kampuni ya Channel One lililokuwa likisafiri kutokea Moshi kuelekea Tanga kugongana uso kwa uso na basi dogo aina ya Coaster lililokuwa likitoka wilayani Same.
Ajali hiyo imetokea katika eneo la Sabasaba kata ya Same, wilayani Same, mkoani Kilimanjaro, na magari yote mawili yamewaka moto.
Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kueleza kuwa juhudi za uokoaji zinaendelea ili kunusuru abiria na kutoa miili ya waliopoteza maisha.