“Ni hatua muhimu katika kuhakikisha huduma ya umeme inaimarishwa ili kuendana na kasi ya maendeleo,” amesema Mpogolo.
Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya alitumia fursa hiyo kupeleka salamu za shukrani kwa Mheshimiwa Rais kwa kushughulikia kwa vitendo changamoto ya maji jijini Dar es Salaam.
“Tupelekee salamu kwa Mheshimiwa Rais kwa kuleta zaidi ya Shilingi bilioni 37 ambazo zimewezesha ujenzi wa tanki kubwa la maji lililopo Bangulo, Wilaya ya Ilala. Tenki hilo litakuwa sehemu muhimu ya kusaidia upatikanaji wa maji kwa wakazi wa jiji na pia litachangia katika upatikanaji wa umeme,” ameongeza.
Vilevile, ameeleza shukrani kwa Serikali kwa kuendelea kupeleka fedha za maendeleo katika wilaya mbalimbali za Dar es Salaam, jambo ambalo limechochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi na kuchangia ustawi wa nchi kwa ujumla.








