Dar es Salaam, 18 Julai 2025
Mwandishi wa vitabu vya kuelimisha watoto, Bi. Riziki Mohamed Juma, amezindua rasmi kitabu chake kipya kiitwacho “Saburi” katika hafla iliyofanyika katika Maktaba Kuu ya Taifa jijini Dar es Salaam.
Uzinduzi huu uliambatana na utambulisho wa vitabu vingine vya watoto, vikiwemo vya maandishi ya kawaida na vya nukta nundu kwa ajili ya watoto wenye mahitaji maalum.

Vitabu hivi vimetolewa kwa ushirikiano kati ya Mtalimbo Books na Dhahabu Publishers, na vinapatikana katika maduka ya vitabu na maktaba za jamii nchini.

Vitabu hivi vimetolewa kwa ushirikiano kati ya Mtalimbo Books na Dhahabu Publishers, na vinapatikana katika maduka ya vitabu na maktaba za jamii nchini.
Saburi ni hadithi ya kuvutia inayowasilisha ujumbe kuhusu athari za utoro shuleni kwa njia rahisi na ya kufundisha. Ni kitabu kinachofaa kwa watoto, wazazi, walezi na walimu.