Dar es Salaam, Julai 2025 – Airtel Africa imetangaza matokeo bora kwa robo ya kwanza iliyoishia Juni 30, 2025, ikionesha ongezeko la wateja wanaotumia huduma za intaneti na Airtel Money katika nchi mbalimbali za Afrika.
Afisa Mtendaji Mkuu, Sunil Taldar, amesisitiza kuwa mafanikio haya ni matokeo ya utekelezaji wa mkakati thabiti unaolenga kuboresha huduma kwa wateja na kuwekeza katika teknolojia mpya kama vile Airtel Spam Alert ili kuhakikisha usalama na kuimarisha imani ya mtandao.
