Simba ilitangulia kumtaka Basiala mapema tu, lakini haikufanya uamuzi wa mwisho kisha juzi, wakarudi na dau la Dola 70,000 wakimtaka kiungo fundi huyo.
Hata hivyo, wakati Maniema wakiweka ngumu kumuachia kiungo huyo kwa dau hilo, Azam imetua ikitaka huduma ya Mkongomani huyo msimu ujao.
Inaelezwa kwamba kocha Florent Ibenge ndiye aliyependekeza usajili wa kiungo huyo anayeweza kucheza nafasi ya kiungo mshambuliaji.
Mwanaspoti iliwahi kuandika kuwa, Simba ilitajiwa bei ya kumpata kiungo huyo, huku ikitakiwa kumnunua kwa Dola 150,000 licha ya wao kutoa kiasi walichotoa.
Kama atatua Azam atacheza nafasi moja na Fei, lakini kama tetesi za Mzenji huyo kwenda Simba au Yanga zikikamilika, Agee atakuwa ndiye mrithi wake.