Nimepata kuwashuhudia walinzi wengi wa kulia wakicheza soka kwenye ardhi hii ya Tanzania hapa nazungumzia wazawa na hata waliokuja wakitokea nje ya Tanzania
Lakini hayupo mlinzi wa kulia mwenye mwendelezo wa kiwango cha juu mechi baada ya mechi kumzidi Shomy , bado pia hayupo beki wa kulia hatari kwenye box la wapinzani kumzidi Kapombe
Kufunga sio jambo geni kabisa kwake , amefunga sana ligi ya ndani , amefunga pia kimataifa akiwa na klabu na bado anafunga Timu ya Taifa
Ukiwa na Shomari unapata uhakika eneo la ulinzi , unakuwa na matumaini ya kushuhudia assist muda wowote kutoka kwake na inapobidi basi anaimaliza mechi mwenyewe kama ilivyotokea hii leo