TIMU ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars imeungana na Kenya kwenye mlango wa kutokea kwenye michuano ya CHAN2024 kufuatia kipigo cha 1-0 dhidi ya Morocco kwenye robo fainali ya michuano hiyo katika dimba la Benjamin Mkapa.
Morocco imeungana na Madagascar kwenye nusu fainali ya michuano hiyo, Madagascar ikifuzu kufuatia ushindi wa penalti 4-3 dhidi ya wenyeji wenza, Kenya kwenye robo fainali.
FT: Tanzania 🇹🇿 0-1 🇲🇦 Morocco
⚽ 65′ Lamlioui