Mshambuliaji wa Tanzania, Kelvin John ‘Mbappe’ amefunga magoli mawili wakati timu yake ya Aalborg (Aab Fc) ya Denmark ikiibuka na ushindi wa 6-1 dhidi ya Marstal/Rise IF kwenye mchezo wa raundi ya pili wa kombe la FA (Denish Cup Sec)
Kwa ushindi huo Aab Fc ambayo inashiriki Ligi daraja la pili Nchini Denmark imetinga hatua ya 16 bora ya michuano hiyo.
Marstal/Rise 1-6 Aalborg Fc
⚽ 67’ Mikkelsen
⚽ 01’ Helenius
⚽ 33’ Helenius
⚽ 36’ Kelvin John
⚽ 57’ Kelvin John
⚽ 65’ Hansen
⚽ 71’ Ross