Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ismail Alli Issu, amesema uwepo wa miradi mingi yenye thamani kubwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu ni kielelezo tosha kwamba usalama kwa sasa si hiari tena bali ni sharti la lazima katika kuendeleza maendeleo.
Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Mhe. Kanali Isaac Mwakisu, amesema kwa kuwa halmashauri hiyo ni mpya, suala la maendeleo linaendana moja kwa moja na uwepo wa ulinzi na usalama wa uhakika.
Kituo cha Polisi Nyakitonto chenye hadhi ya Daraja B kimezinduliwa na mbio za Mwenge wa uhuru
Kituo cha Polisi Nyakitonto chenye hadhi ya Daraja B kimezinduliwa na mbio za Mwenge wa uhuru
Na Fredy Mgunda,Kasulu Kigoma.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ismail Alli Issu, amesema uwepo wa miradi mingi yenye thamani kubwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu ni kielelezo tosha kwamba usalama kwa sasa si hiari tena bali ni sharti la lazima katika kuendeleza maendeleo.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kituo cha Polisi Nyakitonto chenye hadhi ya Daraja B, Issu amesisitiza kuwa mara nyingi panapojengwa vituo vya polisi vya kisasa, basi tambua eneo hilo limepiga hatua kubwa za maendeleo.
“Mkuu wa Wilaya amesema tumejenga kituo hiki kwa sababu uhitaji wake umekuwa mkubwa. Ninyi wenyewe ni mashahidi, miradi yenye thamani kubwa iliyopo hapa Kasulu ndiyo kielelezo cha kasi ya maendeleo,” amesema Issu.
Ameongeza kuwa kutokana na hatua kubwa zilizopigwa, ana uhakika si muda mrefu Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu itapanda hadhi na kuwa Manispaa.Amewataka wananchi kushirikiana katika kulinda amani na usalama ili matarajio hayo yaweze kutimia kwa haraka.
Awali, Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Mhe. Kanali Isaac Mwakisu, amesema kwa kuwa halmashauri hiyo ni mpya, suala la maendeleo linaendana moja kwa moja na uwepo wa ulinzi na usalama wa uhakika.
Kituo hicho cha Polisi Nyakitonto kimejengwa kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri kwa gharama ya shilingi milioni 114 kikiwa ni sehemu ya jitihada za kuhakikisha usalama, amani na utawala wa sheria vinadumu katika wilaya hiyo.