BEKI wa kushoto wa Yanga, Mohamed Hussein Zimbwe Jr ametuma salamu mpya kwa wale wote wanaosema hana furaha tangu ajiunge na kikosi hicho.
Zimbwe aliyetua Yanga katika usajili wa dirisha kubwa msimu huu baada ya kumaliza mkataba ndani ya kikosi cha Simba, alisema anashangazwa na habari hizo, kwani vitu vyote ambavyo huwa anavifanya katika maisha yake anakuwa na malengo anayojiwekea na pale anapoyati-miza huwa anajisikia furaha.
“Hizi habari watu wanazitoa wapi kuwa mimi sina furaha na timu niliyopo? Wao wamekuja? Ni habari mbaya sana na za uchonganishi, mimi naziona tu huko mitandaoni, kwanza kwa nini watu wanisemee kuwa sina furaha? Sasa niwaambie tu kila mtu angependa kuwa mwenye furaha kwa sehemu aliyopo, hivyo mimi nina furaha kama zote kwa mahali nilipo,” amesema Zimbwe baada ya mashabiki mtandaoni kusema amehamia Yanga, lakini hana furaha ma kwamba amepoteza namba mbele ya Chadrack Boka wakati ndani ya Simba alikuwa panga pangua.
“Unajua lengo mojawapo la mwanadamu katika maisha yake hapa duniani ni kuitafuta furaha, kwamba purukushani zote hizi katika maisha zina lengo la kuisaka furaha, kila mtu anapenda kuwa na furaha kwenye maisha yake, vyote tunavyovifanya na malengo tunayoweka na pale tunapoyatimiza huwa tunajisikia furaha, watu waache uzushi wao na wasiwe wasemeji wangu,” amesema Zimbwe Jr.
Hivi karibuni kumezuka mijadala katika mitandao ya kijamii kuwa tangu Zimbwe Jr alipojiunga na Yanga SC, wakidai hana furaha ndani ya timu hiyo kongwe na mabingwa wa kihistoria wa Ligi Kuu Bara.
Zimbwe kutua kwake Yanga msimu huu, kulihitimisha takribani miaka 11 aliyohudumu ndani ya Simba aliyojiunga nayo mwaka 2014 akitokea Kagera Sugar.
Katika kipindi cha miaka 11 akiwa Simba, Zimbwe amekuwa sehemu ya mafanikio makubwa ya kikosi hicho kwa kushinda mataji manne mfululizo ya Ligi Kuu Bara msimu wa 2017-2018, 2018-2019, 2019-2020 na 2020-2021. Pia ameshinda makombe ya FA na Ngao ya Jamii.
Zimbwe pia amechangia Simba kufanya vizuri katika michuano ya CAF, huku timu hiyo ikicheza fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika msimu uliopita 2024-25 na kupoteza mbele ya RS Ber-kane. Kabla ya hapo, imeishia robo fainali za CAF mara tano kuanzia 2018.
Msimu huu baada ya kutua Yanga, Zimbwe ameanza na ubingwa wa Ngao ya Jamii, baada ya kuifunga Simba bao 1-0, huku kikosi hicho kikiwa hatua ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika ku-wania kufuzu makundi.
The post RASMI….ZIMBWE Jr AVUNJA UKIMYA ISHU YA KUTOKUWA NA FURAHA YANGA….ATAJA KILA KITU… appeared first on Soka La Bongo.