Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Patrobas Katambi (katikati) akisikiliza kwa makini mawasilisho mbalimbali katika uzinduzi wa mradi wa Vijana Plus ambao umeratibiwa na Shirika la Save the Children kwa Ushirikiano na Taasisi ya Tanzaniabora Initiative pamoja na Umoja wa Ulaya ambayo imefanyika leo tar 21/3/2025 katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Patrobas Katambi (kushoto) sambamba na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Save the Children Tanzania Angela Kauleni (kulia) wakiwa katika uzinduzi wa mradi wa Vijana Plus ambao umeratibiwa na Shirika la Save the Children kwa Ushirikiano na Taasisi ya Tanzaniabora Initiative pamoja na Umoja wa Ulaya ambayo imefanyika leo tar 21/3/2025 katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Save the Children Tanzania Angela Kauleni katika hafka ya uzinduzi wa mradi wa Vijana Plus ambao umeratibiwa na shirika hilo kwa Ushirikiano na Taasisi ya Tanzaniabora Initiative pamoja na Umoja wa Ulaya ambayo imefanyika leo tar 21/3/2025 katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam.
Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya ambaye pia ni Meneja wa Asasi za Kiraia na Vijana Neema Bwewra akizungumza katika uzinduzi wa mradi wa Vijana Plus ambao umeratibiwa na Shirika la Save the Children kwa Ushirikiano na Taasisi ya Tanzaniabora Initiative pamoja na Umoja wa Ulaya ambayo imefanyika leo tar 21/3/2025 katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi ya Tanzaniabora Initiative Ismail Biro akizunguma katika uzinduzi wa mradi wa Vijana Plus ambao umeratibiwa na Shirika la Save the Children kwa Ushirikiano na Taasisi ya Tanzaniabora Initiative pamoja na Umoja wa Ulaya ambayo imefanyika leo tar 21/3/2025 katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi wa Vijana serikali ya Mapinduzi Zanzibari na Mwakilishi wa Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo Zanzibar Shaibu Muhamad akizungumza katika uzinduzi wa mradi wa Vijana Plus ambao umeratibiwa na Shirika la Save the Children kwa Ushirikiano na Taasisi ya Tanzaniabora Initiative pamoja na Umoja wa Ulaya ambayo imefanyika leo tar 21/3/2025 katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam.
Wasanii wakitoa burudani katika uzinduzi wa mradi wa Vijana Plus ambao umeratibiwa na Shirika la Save the Children kwa Ushirikiano na Taasisi ya Tanzaniabora Initiative pamoja na Umoja wa Ulaya ambayo imefanyika leo tar 21/3/2025 katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam.
Baadhi ya Vijana kutoka taasisi na mashirika mbalimbali walioshirikia katika uzinduzi wa mradi wa Vijana Plus ambao umeratibiwa na Shirika la Save the Children kwa Ushirikiano na Taasisi ya Tanzaniabora Initiative pamoja na Umoja wa Ulaya ambayo imefanyika leo tar 21/3/2025 katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam.
……………………..
NA MUSSA KHALID
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Patrobas Katambi amesema serikali itaendelea kuhakikisha inaongeza fursa za ajira na mitaji kwa vijana ili waweze kujikwamua kiuchumi.
Naibu Waziri Katambi ametoa kauli hiyo jijini Dar es salaam wakati akizungumzia katika uzinduzi wa mradi wa Vijana Plus ambao umeratibiwa na Shirika la Save the Children kwa Ushirikiano na Taasisi ya Tanzaniabora Initiative pamoja na Umoja wa Ulaya ukitarajiwa kutekelezwa katika mikoa zaidi ya saba Tanzania Bara na Zanzibar.
Naibu Waziri amesema mradi huo unalenga kuwawezesha vijana kuwa viongozi bora kwenye taasisi na makampuni na vyombo mbalimbali vya maamuzi.
Aidha Naibu Waziri Katambi amewasisitiza kutambua kuwa wakati ni sasa hivyo wahakikishe wanatumia fursa mbalimbali zinazotolewa na serikali ili waweze kujikwamua kiuchumi.
Awali akizungumzia Mkurugenzi Mkazi wa Save the Children,Angela Kauleni,amesema kuwa takriban vijana 7000 wanatarajia kunufaika na mradi huo.
‘Tukiwawezesha vijana kwa kupitia mafunzo na rasilimali wanazozihitaji wataweza kuzibaini changamoto wanazokabiliana nazo lakini pia watakuwa na ujasiri na ushawishi wa kuishauri serikali na watunga maamuzi na sera ya kwamba ni jinsi gani Tanzania iendele ili kuleta matokeo chanya”amesema Kauleni
Kwa upande wao Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya ambaye pia ni Meneja wa Asasi za Kiraia na Vijana Neema Bwewra amesema kuwa umoja wa ulaya wameweza kifanya mipango kwa kuyasaidia mashirika ya vijana ili kuweza kujiongezea maendelei
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi ya Tanzaniabora Initiative Ismail Biro wamesema kuwa dhamira yao ni kuhakikisha mradi huo unafanikiwa na kuleta matokeo Chanya kwa vijana na taifa kwa ujumla.
Naye Mkurugenzi wa Vijana serikali ya Mapinduzi Zanzibari na Mwakilishi wa Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo Zanzibar Shaibu Muhamad ametumia fursa hiyo kuipongeza Shirika la Save the Children na washirika wengine kuhusu mradi huo na kuahidi kuwa watatoa kila aina ya ushirikiano ili uweze kufanikiwa.