Na Oscar Assenga,Pangani
Akizungumza wakati akizindua mradi huo ambao umetekelezwa kwa muda mfupi kwa kutumia Force Akaunti, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt,Balozi Batilda Burian,Mkuu wa wilaya ya Pangani Gift Msuya alisema utakuwa chachu ya maendeleo kwa wananchi.
Alisema matarajio yao kutokana na utekelezaji wa mradi huo na mengine mikubwa ya maji katika kata za nne za wilaya hiyo na maeneo mengine wana uhakika ifikapo Desemba mwaka huu upatikanaji wa maji utafikia asilimia 90.2.
Alisema hilo linatokana na miradi mikubwa inayotekelezwa, Mkwaja, Sange, Madanga na Bushiri na maeneo maengine wana uhakika kufikia kiwango hicho cha upatikanaji wa maji na kwa upande wa mijini wana miradi miwili ya inayotekelezwa wa hati fungani.
Ambapo alisema mradi huo wa hatifungani ni kuboresha miundombinu ya usambazaji wa maji mjini kwa kuiondosha ya zamani chakavu na kuweka mipya na mradi wa mji 28 ambao uliwekwa jiwe la msingi na Rais Dkt Samia Suluhu alipofanya ziara Tanga.
Alisema kwamba na mradi huo utafanyika kwenye kata kata ya Madanga,Ubangaa na Pangani Mashariki na Magharibu ambapo mpaka sasa upatikanaji wa maji Mijini ni asilimia 76 na mradi utakapokamilika Desemba watakiwa wamefikia upatikanaji wa maji asilimia 100 na kuvuka lengo la utekelezaji wa ilani asilimia 95 kwa upatikani wa maji mijini kwa wilaya ya Pangani.
“Ndugu zangu niwaambie kwamba hakuna mbadala wa maji ndio sababu hakuna maendeleo yanaweza kuja bila kuwepo kwa maji kwa sababu wananchi wakikosa maji hakutakuwa na utulivu wa kiasiasa wala uchumi hivyo uchumi unaonekana kwa sababu huduma za maji zinapatikana na niwapongeze Ruwasa kwa kazi nzuri na juhudi mnazozionyesha kuwapatia wananchi huduma safi ya maji salama na kutosheleza “Alisema
Awali akizungumza kuhusu mradi huo ,Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Tanga Mhandisi Upendo Omari Lugongo alisema kwamba mradi huo ulizinduliwa mwaka jana na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi,Dkt Batilda Burian na mwaka huu ameuzindua mradi huo wa maji ambao miuondombinu yake inaruhusu kuteka maji sio kwenye vilula tu na inaruhusu kuunganisha maji majumbani.
“Kwenye mji huu ambao mradi umezinduliwa kuna kaya zaidi ya 600 na mpaka sasa kaya 20 zimeunganishwa maji kwenye nyumba zao kwa hiyo tunaendelea kuwahamasisha wananchi kuunganisha nyumba kwenye nyumba zao”Alisema
Aidha alisema kwa Mkoa wa Tanga tayari wilaya ya Pangani wamekwisha kutekeleza ilani ya CCM kwa asilimia 100 ambapo hali ya upatikanaji wa maji mpaka sasa ni asilimia 86 lakini kimkoa ni asilimia 75 .
Hata hivyo alisema kwa hiyo wilaya hiyo ilani imetekeleza kwa asilimia 100 na wilaya nyengine wanaendelea na wanatategemea ifikapo Desemba 2025 zaidi ya asilimia 90 wananchi wa Pangani watapata maji safi na salama kwa eneo la Vijijini na Mijini.