Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Methusela Ntonda akisikiliza Maelezo kutoka kwa Bi. Eliafile Solla alipotembelea banda la Mamlaka ya Elimu Tanzania kwenye ufunguzi wa maonesho ya Kazi za Utamaduni na Sanaa.
::::::::::
Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) imepongezwa kwa utekelezaji mzuri wa miradi ya maendeleo ya elimu kupitia Mfuko wa Elimu wa Taifa pamoja na Mfuko wa Kuendeleza Ujuzi (SDF).
Awali, akitoa utambulisho wa Mamlaka hiyo, Afisa Uhusiano na Mawasiliano wa TEA, Bi. Eliafile Solla alisema, TEA ilianzishwa kwa lengo la kusimamia Mfuko wa Elimu wa Taifa, ambapo majukumu yake makuu ni kutafuta rasilimali fedha kutoka kwa wadau wa ndani na nje ya nchi, pamoja na kuzitumia kusaidia juhudi za Serikali katika kuboresha miundombinu ya elimu nchini. Aliongeza kuwa TEA pia ina jukumu la kuratibu na kusimamia utekelezaji wa miradi ya uendelezaji ujuzi kupitia Mfuko wa SDF.
