Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Juni 17, 2025 amemwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kilele cha Maadhimisho ya Miaka 50 ya Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) yanayofanyika katika viwanja vya Taasisi hiyo, Bamaga Jijini Dar es Salaam.
kaulimbiu ya maadhimisho ni _Kitabu Kimoja Mwanafunzi Mmoja, Mpe Kitabu Gusa Ndoto_ .Kaulimbiu hiyo inaunga mkono juhudi za serikali za kuchapa na kusambaza vitabu kwa lengo la kufikia uwiano wa Kitabu kimoja Mwanafunzi mmoja.