Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Ureno Mhe. Marcelo Rebelo de Sousa, mazungumzo yaliyofanyika pembezoni mwa Kikao cha 80 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Jijini New York nchini Marekani.
Mazungumzo hayo yamelenga kuimarisha ushirikiano uliopo baina ya Tanzania na Ureno katika sekta mbalimbali za kimkakati.