Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego (kulia) akichukuliwa picha na Mwendesha Vifaa vya Biyometriki (BVR), Christina Isaya aliyepo Kituo cha Chuo cha Ufundi na Marekebisho kwa watu wenye ulemavu Sabasaba leo Septemba 25,2024 katika siku ya kwanza ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura mkoa wa Singida. Katikati ni Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Dkt Zakia Mohamed Abubakar akishuhudia.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego (kushoto) akiweka saini katika kadi yake ya Mpiga Kura kupitia kishkwambi cha BVR. Mkuu wa Mkoa aliboresha taarifa zake katika Kituo cha Chuo cha Ufundi na Marekebisho kwa watu wenye ulemavu Sabasaba leo Septemba 25, 2024.
Wananchi wakiwa katika vituo vya Uboreshaji Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kuboresha taarifa zao na kujiandikisha katika Daftari hilo mkoani Singida.
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Dkt Zakia Mohamed Abubakar leo ametembelea vituo kadhaa na kushuhudia wananchi mbalimbali wakijiandikisha na kuboresha tarifa zao katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.