Na Diana Byera,Missenyi.
Jumla ya Milioni Tatu zinashindaniwa katika Mashindano ya mpira wa miguu yaliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Nkenge wilaya Missenyi mkoani Kagera ambayo yatashirikisha timu 20 kutoka katika wilaya hiyo.
Mashindano hayo yenye jina la Dk.Samia Na Kyombo yanalenga kuwakunsanya vijana wa wilaya ya Missenyi ili kuibua vipaji vya vijana wanaoishi vijiji vya pembezoni mwa Tanzania na kiviendeleza katika ngazi nyingine za mpira wa miguu chini pamoja na kuendeleza mshikamano kutoka kwa vijana wa kata moja Hadi nyingine
Mashindano hayo yamefunguliwa Rasmi na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa katika Uwanja wa Mashujaa, Bunazi, wilayani Missenyi, mkoani Kagera, na Yanatarajia kutamatika Juni mwaka huu baada ya kupata timu ambazo zitaingia Fainali.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Waziri Bashungwa alisema kuwa mashindano hayo yatasaidia kuibua vipaji vya michezo kwa vijana, kuimarisha afya, kuendeleza mshikamano na kudumisha upendo miongoni mwa vijana na wakazi wa Wilaya ya Missenyi huku watakaonyesha vipaji vyao watapata nafasi ya kutafuta Fursa nyingine Za kimichezo ndani na nje ya nchi
“Mbunge kwa kushirikiana na Madiwani wameonyesha dhamira ya dhati katika maendeleo ya michezo ndani ya Wilaya ya Missenyi Ligi hii siyo tu burudani bali pia ni fursa kwa vipaji chipukizi,wilaya hii Iko pembezoni lakini naelewa kuwa vijana wengi wanavipaji hivyo wasisite kuonyesha vipaji vyao ,naomba vijana kutoka kata zote 20 mshiriki kwa moyo wa upendo na mshikamano,” alisema Bashungwa.
Aidha, Waziri Bashungwa ametoa wito kwa waamuzi na wasimamizi wa mashindano hayo kuhakikisha wanatenda haki wakati wa michezo yote, katika Mashindano hayo ili kiyafanya yamalizike kwa amani na kutimiza malengo yaliyokusudiwa.
Mbunge wa Jimbo la Missenyi, Florent Kyombo, alisesema kuwa mashindano hayo yanalenga kuimarisha mahusiano na mshikamano kati ya vijana na wananchi wa kata zote 20 za wilaya hiyo na hiyo ilikuwa moja ya haadi zake katika kuhakikisha anatekeleza ilani ya chama Cha mapinduzi ni lazima vijana wapate Fursa ya kushiriki michezo na kuonyesha vipaji vyao.
Alisema kuwa viwanja vya Mugana B na uwanja wa Mashujaa Bunazi ndivyo vitakavyotumika katika Mashindano hayo kwa kukutanisha makundi yaliyopangwa na kamati.
Hafla ya uzinduzi ilizikutanisha timu za kata za Kyaka na Mtukula, timu zote shiriki zilipatiwa vifaa mbalimbali vya michezo, ikiwemo jezi, mipira, vifaa vya mazoezi, pamoja na fedha kwa ajili ya maandalizi ya mechi.