Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili Julius Mtatiro.
Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog
Umoja wa Wastaafu Tanzania (Retirees’ Association of Tanzania – REAT) umezinduliwa rasmi katika Mkoa wa Shinyanga kwa lengo la kushughulikia maslahi, haki na ustawi wa wastaafu nchini.
Uzinduzi huu umefanyika leo Jumatatu Mei 26,2025 katika Ukumbi wa CCM Mkoa wa Shinyanga na kuhudhuriwa na wastaafu zaidi ya 700 kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa wa Shinyanga.
Mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili Julius Mtatiro, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mheshimiwa Anamringi Macha.
Akizungumza katika uzinduzi huo, Mtatiro amewahakikishia wastaafu kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan itaendelea kushughulikia changamoto zinazowakabili wazee na kuwashirikisha katika masuala mbalimbali ya maendeleo ya taifa.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili Julius Mtatiro.
“Wazee msiishie tu kusema mnataka kushirikishwa. Tajeni maeneo mnayotaka kushirikishwa. Mnaweza kuanzisha vikundi mkapata mikopo, mkaanzisha miradi yenu. Serikali hii ni sikivu na inafanya kazi kubwa kuboresha maisha ya wananchi,” amesema Mtatiro.
Aidha Mtatiro amewataka wazee kuwa mstari wa mbele katika kudhibiti mmomonyoko wa maadili, hasa vitendo vya ukatili wa kijinsia kama ubakaji na ulawiti ambavyo vinafanyika hata ndani ya familia.
Amesisitiza umuhimu wa malezi bora na tahadhari katika malezi, ikiwa ni pamoja na watoto kutolala chumba kimoja na wageni.
Pia amewasihi wazee kuandika wosia akisema kuwa kitendo hicho si uchuro bali ni maandalizi muhimu ya maisha baada ya wao kuondoka.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili Julius Mtatiro.
“Kuandika wosia si kujichulia kifo. Ni tahadhari na upendo kwa familia zenu. Pia nawaomba wazee tujiepushe na kuanzisha miradi mikubwa isiyoendana na uwezo au uzoefu wetu, na wanaume ambao wake zao wamefariki, tafadhali epukeni kuoa hovyo hovyo. Maisha ya uzeeni yanahitaji utulivu,” ameongeza Mtatiro.
Ameongeza kuwa baadhi ya wazee hujiongezea matatizo kwa kuanzisha miradi au ndoa mpya bila maandalizi ya kutosha, jambo linaloweza kuhatarisha afya na maisha yao.
Katika hatua nyingine amewaomba wazee kuwakumbusha vijana umuhimu wa kulinda amani ya nchi na kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu 2025.
“Naomba wazee tuendelee kuwakumbusha vijana wetu kuwa amani ya nchi inatakiwa kulindwa. Taifa la Tanzania linaendelea kupiga hatua kubwa za kimaendeleo kutokana na utulivu uliopo. Waambieni vijana kuwa tuna taifa moja lenye amani, tunahitaji kulinda taifa hili na kwamba changamoto za taifa hili zinatakiwa kutatuliwa ndani ya taifa hili siyo kutatuliwa na watu kutoka nje ya nchi”,amesisitiza Mtatiro.
Rais wa REAT, Alhaj Dauda Bilikesi.
Kwa upande wake, Rais wa Umoja wa Wastaafu Tanzania (REAT), Alhaj Dauda Bilikesi, amesema lengo kuu la kuanzishwa kwa REAT ni kuimarisha mshikamano wa wastaafu nchini, kutambua mchango wao kwa taifa na kuweka misingi imara ya utetezi wa haki na maslahi yao baada ya utumishi katika sekta ya umma au binafsi.
“Wastaafu ni hazina ya maarifa, uzoefu na hekima. Umoja huu ni jukwaa muhimu la kuhakikisha wastaafu wanaendelea kuheshimiwa na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa hata baada ya utumishi wao,” amesema Alhaj Mbilikesi.
Akisoma risala ya REAT, Mwalimu Mstaafu Magdalena Faustine ameeleza kuwa Umoja huo umejikita katika kuwaunganisha wastaafu wote, kushirikiana na Serikali katika kutetea haki zao, pamoja na kuwahamasisha kushiriki katika shughuli za kijamii na kiuchumi, kutoa elimu kuhusu haki za wastaafu, na kujifunza kutoka kwa taasisi za kimataifa ili kuboresha huduma za wastaafu nchini.
Mwalimu Mstaafu Magdalena Faustine akisoma risala
Amezitaja changamoto zinazowakabili wastaafu kuwa ni pamoja na ucheleweshaji wa mafao, ugumu wa kupata haki kwa wakati, ukosefu wa huduma bora za afya, kutokuwepo kwa vituo vya malezi ya wazee, na kutokuwepo kwa mfumo wa kupandisha pensheni kulingana na mfumuko wa bei. Aidha, alisema wastaafu wengi wanakosa ushirikishwaji katika maamuzi ya kitaifa na kimkoa.
Kwa upande wake, Mratibu Mkuu wa REAT, Mwalimu Ezekiah Oluoch, amesema umoja huo ulioanzishwa mwaka 2021 unawahusisha wastaafu wote wa sekta ya umma na binafsi, bila kujali kada au cheo walichokuwa nacho kabla ya kustaafu, ilimradi wanapokea mafao kupitia mifuko ya hifadhi ya jamii ya PSSSF, NSSF na Hazina.
Mratibu Mkuu wa REAT, Mwl. Ezekiah Oluoch.
“Tunawaomba viongozi wa Serikali wawashirikishe wastaafu katika shughuli za maendeleo ya taifa. Tumestaafu lakini hatujachoka. Hata katika uchaguzi mkuu huu, tunaweza kugombea nafasi mbalimbali kama udiwani na ubunge,” amesema Oluoch.
Katika mapendekezo yao kwa Serikali, Umoja wa Wastaafu Tanzania umependekeza Kuanzishwa kwa mfumo rasmi wa kupandisha pensheni kulingana na mfumuko wa bei, kuongezwa kwa kiwango cha chini cha pensheni kutoka Shilingi 50,000 hadi angalau Shilingi 200,000 kwa mwezi na Serikali kuangalia upya utozwaji wa kodi kwa wazee wenye umri wa miaka 60 na kuendelea.
Mapendekezo mengine ni kuanzishwa kwa mikopo maalumu kwa wastaafu wenye uwezo wa kujishughulisha, huduma bora za afya kupatikana kwa wastaafu kupitia mifuko kama NHIF, kuwashirikisha wastaafu katika kutoa ushauri kitaifa kupitia majukwaa rasmi na kuanzishwa kwa ofisi ya REAT Mkoa wa Shinyanga kwa ajili ya uratibu wa karibu wa masuala ya wastaafu.
Baadhi ya wastaafu waliohudhuria uzinduzi huo wamesema wamefurahishwa na kuanzishwa kwa umoja huo kwa kuwa sasa wana jukwaa rasmi la kuwasilisha maoni yao, kutetea haki zao, na kushiriki katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi na kwamba hii ni hatua muhimu ya kuimarisha heshima, utu na usalama wa maisha ya wastaafu.
TAZAMA PICHA HAPA CHINI
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili Julius Mtatiro, akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Anamringi Macha wakati wa uzinduzi wa Umoja wa Wastaafu Tanzania (Retirees’ Association of Tanzania – REAT) katika Mkoa wa Shinyanga leo Mei 26,2025. Picha zote na Kadama Malunde – Malunde 1 blog
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili Julius Mtatiro, akizungumza wakati wa uzinduzi wa Umoja wa Wastaafu Tanzania (Retirees’ Association of Tanzania – REAT) katika Mkoa wa Shinyanga
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili Julius Mtatiro, akizungumza wakati wa uzinduzi wa Umoja wa Wastaafu Tanzania (Retirees’ Association of Tanzania – REAT) katika Mkoa wa Shinyanga
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili Julius Mtatiro, akizungumza wakati wa uzinduzi wa Umoja wa Wastaafu Tanzania (Retirees’ Association of Tanzania – REAT) katika Mkoa wa Shinyanga
Wastaafu wakiwa ukumbini wakati wa uzinduzi wa Umoja wa Wastaafu Tanzania (REAT) katika Mkoa wa Shinyanga
Rais wa REAT, Alhaj Dauda Bilikesi, akizungumza wakati wa uzinduzi wa Umoja wa Wastaafu Tanzania (Retirees’ Association of Tanzania – REAT) katika Mkoa wa Shinyanga
Mratibu Mkuu wa REAT, Mwalimu Ezekiah Oluoch akizungumza wakati wa uzinduzi wa Umoja wa Wastaafu Tanzania (Retirees’ Association of Tanzania – REAT) katika Mkoa wa Shinyanga
Mratibu Mkuu wa REAT, Mwalimu Ezekiah Oluoch akizungumza wakati wa uzinduzi wa Umoja wa Wastaafu Tanzania (Retirees’ Association of Tanzania – REAT) katika Mkoa wa Shinyanga
Katibu Mkuu wa REAT, Mchungaji Emmanuel Samara akizungumza wakati wa uzinduzi wa Umoja wa Wastaafu Tanzania (Retirees’ Association of Tanzania – REAT) katika Mkoa wa Shinyanga
Mjumbe wa Kamati ya Utendaji REAT Taifa na Mratibu wa REAT Taifa Bi. Tabu Mambo akizungumza wakati wa uzinduzi wa Umoja wa Wastaafu Tanzania (Retirees’ Association of Tanzania – REAT) katika Mkoa wa Shinyanga
Wastaafu wakiwa ukumbini wakati wa uzinduzi wa Umoja wa Wastaafu Tanzania (REAT) katika Mkoa wa Shinyanga
Wastaafu wakiwa ukumbini wakati wa uzinduzi wa Umoja wa Wastaafu Tanzania (REAT) katika Mkoa wa Shinyanga