Mkaguzi wa Bidhaa za Petroli EWURA, Mhandisi Mbarouk Shaame akiwasilisha mada kuhusu matumizi sahihi na salama kwa Mama Lishe, Waendesha Bodaboda, Wajasirianali na Wasambazji wa Gesi ya kupikia mkoani Iringa
…
MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imeendelea kutoa hamasa kwa wadau mbalimbali mkoani Iringa kutumia gesi ya kupikia (LPG) ambayo ni nishati safi, ya uhakika na inayotunza afya na mazingira.
Mkaguzi wa bidhaa za Petroli EWURA Mhandisi Mbarouk Shaame, akitoa mada kwa mama lishe, waendesha bodaboda, wauzaji na wasambazaji wa LPG mkoani Iringa.
Pia alisisitiza kuwa EWURA huhakikisha vigezo vya usalama wakati wa uagizaji, uhifadhi, usambazaji na usafirishaji wa gesi ya kupikia vinazingatiwa ili nishati hiyo isilete madhara kwa watu, mali na mazingira.
Mhandisi Shaame alieleza kuwa, EWURA husimamia mlolongo mzima wa biashara ya gesi ya kupikia (LPG)nchini kwa kushirikiana na taasisi nyingine ikiwemo NEMC, TBS na Wakala wa Vipimo ili kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji na upatikanaji wa nishati hiyo huku ikichagiza utekelezaji wa mkakati wa kitaifa wa nishati safi ya kupikia.
Akihitimisha semina hiyo, Meneja wa EWURA Kanda ya Kati, Mhandisi Hawa Shani Lweno, alitoa mwito kwa watanzania kuchangamkia fursa ya biashara ya kusambaza gesi ya kupikia(LPG) ili kusogeza huduma hususani katika maeneo ya pembezoni, ambapo alisiitiza kuwa EWURA hutoa leseni na vibali kwa njia rahisi na rafiki kupitia mfumo wa kieletroni wa LOIS.
Mkaguzi wa Bidhaa za Petroli EWURA, Mhandisi Mbarouk Shaame akiwasilisha mada kuhusu matumizi sahihi na salama kwa Mama Lishe, Waendesha Bodaboda, Wajasirianali na Wasambazji wa Gesi ya kupikia mkoani Iringa
Mkaguzi wa Bidhaa za Petroli EWURA, Mhandisi Mbarouk Shaame akiwasilisha mada kuhusu matumizi sahihi na salama kwa Mama Lishe, Waendesha Bodaboda, Wajasirianali na Wasambazji wa Gesi ya kupikia mkoani Iringa
Mkaguzi wa Bidhaa za Petroli EWURA, Mhandisi Mbarouk Shaame akiwasilisha mada kuhusu matumizi sahihi na salama kwa Mama Lishe, Waendesha Bodaboda, Wajasirianali na Wasambazji wa Gesi ya kupikia mkoani Iringa.
Afisa Habari Jeshi la Zimamoto mkoani Iringa,Zmm 0145 Fc Adolf Kameya,akitoa elimu ya kukabiliana na moto wa gesi ya kupikia kwa mama lishe, dereva bodaboda, wajasiriamali na wasambazaji wa bidhaa hiyo wakati wa semina ya EWURA kwa wadau hao.
Afisa Habari Jeshi la Zimamoto mkoani Iringa,Zmm 0145 Fc Adolf Kameya,akitoa elimu ya kukabiliana na moto wa gesi ya kupikia kwa mama lishe, dereva bodaboda, wajasiriamali na wasambazaji wa bidhaa hiyo wakati wa semina ya EWURA kwa wadau hao.