Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika viwanja vya Stendi ya Mabasi Meatu kwa ajili ya kuzungumza na wananchi katika muendelezo wa Ziara yake ya Kikazi mkoani Simiyu tarehe 17 Juni, 2025.
Sehemu ya Wananchi wa Meatu waliohudhuria mkutano wa hadhara wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan uliofanyika katika viwanja vya Stendi ya mabasi tarehe 17 Juni, 2025.