RAIS Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Bw. Ngusa Samike, aliyekuwa Katibu wa Rais wa Awamu ya Tano Marehemu Dkt John Pombe Magufuli aliyefika kumjulia hali ofisini kwake Masaki jijini Dar es salaam Jumatatu Julai 14, 2025.
Bw Samike alikuwa Katibu wa Dkt Magufuli toka marehemu alipokuwa Waziri. Pia amewahi kuwa RAS wa jiji la Mwanza, hivi sasa anajishughulisha na kilimo na ufugaji kwao Sengerema.
