Meneja wa Chama cha akiba na mikopo Mahanje Saccos Kassim Masengo,akizungumza jana ofisini kwake kuhusu mafanikio ya chama hicho katika kipindi cha miaka minne cha Serikali ya awamu ya sita.
Baadhi ya Wanachama wa Chama cha akiba na mikopo Mahanje Saccos Halmashauri ya Madaba Mkoani Ruvuma wakipata huduma mbalimbali za mikopo na fedha kwenye Chama chao.
Meneja wa Chama cha akiba na mikopo Mahanje Saccos Kasim Masengo kulia na baadhi ya wakulima ambao ni wanachama wa chama hicho wakimsikiliza Afisa Ushirika wa Halmashauri ya Madaba Wilayani Songea Sadam Fupi aliyetembelea moja ya shamba la mkulima wa mahindi katika kijiji cha Madaba
Mkulima wa zao la mahindi ambaye ni Mwanachama wa Chama cha akiba na mikopo Mahanje Saccos ambaye hakufahamika jina lake mara moj kushoto,akimuonyesha Afisa Ushirika wa Halmashauri ya Madaba Wilayani Songea Sadam Fupi sehemu ya shehena ya mahindi aliyozalisha katika msimu wa kilimo 2024/2025,katikati Meneja wa Mahanje Saccos Kasim Masengo.
Na Mwandishi Wetu,Madaba
Alisema, asilimia kubwa ya wakulima wake wanajihusisha na kilimo cha zao la mahindi,maharage na mpunga na zao la mahindi soko kubwa ni la Serikali kupitia Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula(NFRA)Kanda ya Songea na kwa muda wa miaka minne wameuza zaidi ya tani 90.
Alisema,awali walipata shida kwenye uzalishaji kwani upatikanaji wa mbolea ulikuwa mgumu kwa sababu mbolea ilikuwa inauzwa kwa bei kubwa ambayo wakulima wengi walishindwa kumudu gharama zake.