Na Albano Midelo,Songea
Amesema fedha hizo zimetolewa na serikali chini ya Uongozi wa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ambaye amedhamiria kila Mkoa hapa nchini uwe na Chuo Kikuu,hii ni ahadi ambayo aliitoa kwa wananchi na sasa anaitekeleza kwa vitendo kwa wananchi wa Mkoa wa Ruvuma’’,alisema Dkt.Mashaka.
Dkt. Mashaka amesema kuwa chuo hicho kinalenga kuhakikisha wanafunzi wanajifunza kwa vitendo, hasa namna ya kuanzisha na kuendesha biashara ambapo ameeleza kuwa wanataka wanafunzi wao wasitegemee ajira pekee, bali wawe na uwezo wa kujiajiri na kuendesha maisha yao.
Kwa upande wake, Afisa Uhusiano wa IAA Kampasi ya Songea, Nuru Meshack, ameelezea changamoto kubwa waliyoibaini katika Wilaya ya Songea ni wazazi wengi kuamini kuwa mtoto aliyepata daraja la nne hawezi kuendelea na masomo, hivyo amewahimiza wazazi na wanafunzi kuwa ufaulu wa D nne, isipokuwa kwa masomo ya dini, unaruhusu mwanafunzi kujiunga na chuo.
Amewakaribisha wanafunzi kujiunga na IAA Kampasi ya Songea, akisisitiza kuwa chuo hicho kimejikita katika kuwasaidia wanafunzi kujiajiri badala ya kutegemea kuajiriwa na mazingira ya kusomea ni mazuri na yanasaidia mwanafunzi kufanikisha malengo ya kielimu na kuendana na teknolojia.
Chuo cha Uhasibu Arusha Kampasi ya Songea kinapatikana katika jengo la TTCL, ghorofa ya pili, karibu na ofisi za Manispaa ya Songea. Kwa mawasiliano zaidi namba 0784-171-565 au kufika moja kwa moja kwenye ofisi zao.
