Kampuni ya Puma Energy Tanzania imetangaza uzinduzi rasmi wa kituo cha umeme wa jua chenye uwezo wa kilowati 570 katika kiwanda cha tumbaku cha Alliance One Tanzania Tobacco Limited (AOTTL).
Kituo hiki cha kisasa kinajumuisha paneli za sola 1,296 na inverter 6 zenye ufanisi wa hali ya juu. Mfumo huu uliounganishwa na gridi ya taifa umetengenezwa kutoa umeme wa kutosha wakati wa mchana kipindi chote cha uzalishaji wa kiwanda kuanzia Mei hadi Oktoba.
Bi. Fatma Abdallah, Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania, alisema “Mradi huu wa sola katika kiwanda cha Alliance One ni mafanikio makubwa, si tu kwa Puma Energy bali pia kwa sekta ya viwanda Tanzania.
Ikiwa na dhamana ya utendaji wa miaka 30, mfumo huu wa sola unahakikisha ufanisi wa nishati wa muda mrefu na uendelevu wa mazingira. Ni ushahidi thabiti wa maono ya Puma Energy ya kuwezesha sekta ya viwanda Tanzania kupitia suluhisho la nishati safi, bunifu, na imara, kwa ajili ya kukuza uchumi unaokwenda sambamba na utunzaji wa mazingira.