MAHAKAMA Kuu ya Tanzania imekizuia chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kufanya shughuli zozote zile za kisiasa na kutumia mali zake mpaka pale kesi ya msingi namba 8323/2025 iliyofunguliwa na aliyewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Zanzibar, Said Issa na wenzake wawili itakaposikilizwa na kutolewa uamuzi.
Uamuzi huo umetolewa leo na Jaji Hamidu Mwanga. huku CHADEMA ikikosa muwakilishi wa kisheria baada ya Wakili wake, Jebrah Kambole aliyekuwa akisimamia kesi hiyo kujitoa kabla ya kutolewa uamuzi akidai kutosikilizwa kwa hoja zao.