Ujumbe kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali wakiongozwa na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Samwel M. Maneno wamekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa PSSSF Dkt. Rhimo Nyansaho na baadhi ya Wafanyakazi wa mfuko huo, mazungumzo baina ya Taasisi hizo yamelenga kubadilishana uzoefu katika eneo la Huduma kwa Wateja.
Ujumbe huo umekutana na PSSSF tarehe 24 Julai, 2025 katika Makao Makuu ya Mfuko wa PSSSF Jijini Dodoma.
Katika kikao hicho Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali aliambatana na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Bi. Leila Muhaji, Wakili wa Serikali Mkuu Dkt. Jaba Shedrack, Afisa TEHAMA Mwandamizi Bw. Juma Mziray na Wakili wa Serikali Bw. Nyamhanga Nyamhanga.